Saturday, January 26, 2013

Nigeria Vs Zambia


R Kelly - Storm is over


Matunda ya Yanga Uturuki yajibu Taifa

IKICHEZA soka lenye ‘harufu’ ya Uturuki, Yanga jana iliwathibitishia mashabiki wake ilichojifunza Ulaya baada ya kuiogesha kichapo cha mabao 3-2 Leopards  ya Afrika Kusini katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Yanga ilirejea nyumbani mwanzoni mwa wiki hii baada ya wiki mbili za kujifua nchini Uturuki ilikocheza mechi tatu, ikifungwa mbili na sare moja.
Jana Yanga ilikuwa tofauti na ilivyozoeleka awali kufuatia kuonyesha soka lenye ‘taaluma’ na kuwapeleka puta Chui kutoka Bondeni.
Chanzo:  mwananchi